KARIBUNI MCHICHANI

Kwa Habari moto moto Kuhusu Siasa , Uchumi, Maisha, Elimu Na Mengine Mengi.



Tuesday, September 14, 2010

JUMBA LA BIG BROTHER - MAJI SHINGONI MWISHO NA KIMWANA CHA NAMIBIA, APUMUA KWA MASHINE.

Mshiriki wa shindano la Big Brother kutoka Tanzania, Mwisho Mwampamba akiwa an rafiki yake Uti kutoka Nigeria.
Mshiriki wa shindano la Big Brother kutoka Tanzania, Mwisho Mwampamba, amenusurika
kutolewa katika jumba hilo, ambalo juzi Jumapili lilishuhudua mwanadada wa Zambia, Paloma, akitupwa Zizizini
Kwa mujibu wa kanuni mpya ya shindano hilo mwaka huu, washiriki wakitolewa kwenye Jumba la Big Brother, hupelekwa kwenye Zizi, ambako wanaishi pamoja na wanyama walio hai kama ng'ombe na kuku.
Hata hivyo, washiriki waliobaki kwenye nyumba kuu ya Big Brother, hawana ufahamu wowote kama wakitolewa watapelekwa zizini, na kila atokaye hushangaa kuona kwamba wenzake wote waliotolewa awali wanaishi kwenye zizi.
Mtangazaji wa shoo wa kutolewa kwa washiriki kwenye jumba hiloMshiriki wa shindano la Big Brother kutoka Tanzania, Mwisho Mwampamba akiwa an rafiki yake Uti kutoka Nigeria., IK, alisema juzi kuwa baada ya wiki tatu zijazo, washiriki "angalau wawili watarejeshwa kwenye nyumba kuu" katika kuthibitisha kauli kwamba hata washiriki waliopelekwa zizini bado wamo mchezoni na wanayo nafasi ya kutwaa zawadi ya kwanza ambayo ni dola 200,000 (sawa na Sh. Milioni 295 za Tanzania).

Hii ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Mwisho kupigiwa kura ya kutoka mjengoni humo. Mara ya kwanza alipopendekezwa na wenzake, alikuwa kiongozi ya nyumba wa wiki hivyo, alipotakiwa kutumia madaraka yake kumuokoa mmoja na kumpachika mwingine katika 'chekeche' la kupigiwa kura na watazamaji, alijiokoa mwenyewe na kumuweka kijana anayeonekana kukubalika zaidi, Munya, kutoka Zimbabwe.
Munya amethibitisha kuwa anapendwa sana na Waafrika ambao ndio hupiga kura kwa njia ya simu na internet, baada ya kunusurika mara sita, ambapo kila aliyewekwa na kijana huyo kwenye 'chekeche,' alitupwa nje.
Hali hiyo ilimfanya mshiriki kutoka Ethiopia, Yacob, kumuita Munya kuwa "Bingwa Mtetezi" wakati walipowekwa pamoja kwenye chekeche.
"Munya ndiye bingwa mtetezi, ameshawabwaga 'mabondia' watatu, pambano la wiki hii ni kati yangu na yake, nataka kuona itakuwaje," alisema Muethiopia huyo, ambaye kama ndoto zake zilivyokuwa naye alibwagwa.

Hata hivyo, Yacob, hayumo tena kwenye mashindano hayo baada ya kukaa kwa wiki chache zizini na kisha kumuomba Big Brother amruhusu aondoke mchezoni kwa imani yake kwamba ukiwekwa zizini, inamaanisha kuwa kuna wenzako wenye nafasi zaidi yako ya kushinda tuzo hiyo na kwamba kuendelea kukaa zizini ni kupoteza muda.
Mwisho ameendelea kujivinjari na kimwana wake Mnamibia, Meryl.

CHANZO: NIPASHE

No comments:

Post a Comment